TANGAZA NA BLOG HII KWA GHARAMA NAFUU

TANGAZA NA BLOG HII KWA GHARAMA NAFUU

Wednesday, 28 January 2015

Mabomu yarindima Dar:Ni wakati polisi wakizuia maandamano ya CUF

Mabomu yarindima Dar:Ni wakati polisi wakizuia maandamano ya CUF

Dar es Salaam. Polisi jijini Dar es Salaam jana walifyatua mabomu ya machozi kutawanya viongozi na wafuasi wa CUF na baadaye kumtia nguvuni Profesa Ibrahim Lipumba na wanachama 32, tukio lililosababisha Ukawa kuunganisha nguvu kuwasaidia kuandika maelezo.
Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba, akiwa chini ya ulinzi wa Polisi Dar es Salaam jana, baada ya kukamatwa kwa yeye na wafusi 36 wa Chama hicho 32 madai ya kuandamana bila kibali cha polisi, kukumbuka mauaji ya wafuasi 22 wa Chama hicho huko Pemba, Januari 26 na 27 , 2001 baada ya polisi kupambana na waandamanaji. Picha na Saidi Khamis.
Profesa Lipumba na viongozi wenzake walikuwa wakienda Zakhem, Mbagala kuwatawanya kwa amani wafuasi wa CUF baada ya Jeshi la Polisi kutoa taarifa mapema jana ya kuzuia maandamano na mkutano wa hadhara uliopangwa kwa ajili ya kuadhimisha miaka 14 tangu wafuasi wa chama hicho walipouawa kwa risasi na polisi wakati wakiandamana kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar mwaka 2001. Maandamano hayo yalipangwa kuanzia Temeke Mwisho na kuishia Mbagala Zakhem wilayani Temeke ambako chama hicho kina nguvu kubwa.
Lakini azima yao ilikumbana na mkono wa dola baada ya polisi kuwazuia viongozi hao eneo la Mtoni Mtongani na baadaye kutumia nguvu kutawanya wananchi.
Katika sakata hilo, polisi waliwaweka chini ya ulinzi viongozi wote akiwamo Profesa Lipumba na wafuasi hao walipokuwa wakijiandaa kwenda Viwanja vya Zakhem, ambako mkutano ungefanyika.
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam ilithibitisha kukamatwa kwa Lipumba na wanachama 32 wa CUF kwa kufanya maandamano haramu na walikuwa Kituo Kikuu cha Polisi, ambako viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) walienda pamoja na wanasheria waliotakiwa kuwasaidia kuandika maelezo.

No comments:

Post a Comment